FAHAMU MUDA WA KUSUBIRIA MAJIBU YA VIPIMO MBALIMBALI YA MAABARA UKIWA HOSPITALI



Habari za leo ndugu msomaji wa makala hii?

Mimi ni mzima wa afya, Namshukuru sana Mungu kwa kunilinda na kuniongoza ili niweze kukufahamisha kuhusu muda unaotakiwa kuutumia wakati unasubiri majibu yako maabara.

Maabara kuna vipimo vya aina mbalimbali vinavyoweza kupimwa Maabara na lengo kubwa la mgonjwa kupimwa ni kupata matibabu sahihi.

Orodha ya vipimo niliyoandika hapa chini na muda wa kusubiria vinategemeana na Hospitali husika na idadi ya wahudumu (Wataalamu wa maabara) wanaohudumia, kwa hiyo ni vizuri kwa kila Hospitali kuweka wazi muda wa kusubiria majibu ya kila kipimo wanachopima (vyote)
 
Hapa ni baadhi ya vipimo ambavyo vinapimwa Maabara ni:



AINA YA KIPIMO
MUDA WA KUSUBIRIA MAJIBU
Fully blood count (FBC) (Ni kipimo kinachotumika kupima magonjwa mengi yanayoweza kutokea kwenye damu kama kansa, n.k.)
Masaa manne 4
Haemoglobin (Wingi wa damu)
Dakika 20 hadi 30
Sick ling test (Kupima ugonjwa wa Sickle Cell)
Masaa 24
CD4
Masaa 24
Blood Slide (B/S) (Kipimo cha damu cha kuangalia malaria kwenye damu kwa kutumia darubini)
Saa moja.
Malaria Rapid Diagnostic Test (mRDT) (Kipimo cha damu ili kuangalia malaria kwa kutumia kipimo maalumu cha haraka
Dakika 20 hadi 30
Urine microscopy (Kipimo cha mkojo)
Saa moja.
Stool microscope (Kipimo cha haja kubwa)
Saa moja.
Blood group and Rhesus factor (Kipimo cha kuangalia kundi la damu)
dakika 20 hadi 40
Cross match (Kipimo cha kuangalia ulinganifu wa damu kati ya
Saa moja
VDRL/RPR (Kipimo cha damu ili kuangalia uwepo wa magonjwa ya zinaa)
masaa mawili.
Widal (ext ended) test (Kipimo cha damu ili kuangalia uwepo wa Homa ya matumbo yaani Typhoid)
Masaa 24.
Cryptococcus neo. test
masaa 2
Pregnancy test (Kipimo cha kuangalia ujauzito kwenye mkojo)
Dakika 15 hadi 40.
HIV test
Dakika 30.
Urine for culture (Kuotesha wadudu walio kwenye mkojo)
Siku 3
Stool for culture (Kuotesha wadudu kwenye Haja kubwa au kinyesi)
Siku 4
Urethral and HVS for culture (Kuotesha wadudu kwenye majimaji ya kwenye uti wa mgongo)
Siku 3
CSF for bacteriological test (Kipimo cha majimaji ya kwenye uti wa mgongo ili kuangalia uwepo wa Bakteria)
Masaa 4 hadi 72
Gram stain (Kipimo cha kuangalia kama kuna bakteria kwenye aina yoyote ya kipimo)
Saa moja.
 Sputum for AFB (Makohozi)
Masaa 24hrs hadi 48.
ASAT (Kipimo cha damu ili kuangalia kama ini linafanya kazi vizuri)
Masaa 6 hadi 24
ALAT (Kipimo cha damu ili kuangalia kama ini linafanya kazi vizuri)
Masaa 6 hadi 24
Criatinine (Kipimo cha damu ili kuangalia kama figo zinafanya kazi vizuri)
Masaa 6 hadi 24
Glucose (Kipimo cha sukari kwenye damu)
Masaa 6 hadi 24
CSF Glucose (Majimaji ya kwenye uti wa mgongo ili kutambua kama kuna sukari ndani yake)
Saa moja hadi masaa 6.
Urine for urinalysis (Kipimo cha mkojo ili kuangalia vipimo mbalimbali kama protein, Sukari, Albumin n. k.)
Saa moja.

Maoni

  1. Nataka kutoa ushuhuda kuhusu jinsi nilivyopona kutokana na Virusi vya Herpes. Miezi michache iliyopita nilikuwa na dalili kadhaa. Nilienda kumuona daktari na vipimo vingi vya damu vilifanywa kwangu, baadaye niliambiwa nilikuwa na Herpes. Daktari wangu aliniambia kwamba hakuna tiba ya Herpes. Nilijisikia vibaya, niliingia mtandaoni nikitafuta tiba inayowezekana ya Virusi vya Herpes, niliona chapisho la Dkt. Dawn, daktari wa mitishamba anayewasaidia watu kupona kutokana na Herpes. Saratani. VVU na mengineyo. Niliwasiliana naye na kumwambia jinsi ninavyohisi. Alisema dawa yake ya mitishamba inaweza kuniponya. Alinitumia dawa kupitia huduma ya utoaji wa UPS na nilipokea dawa siku 6 baada ya kuituma, nilichukua dawa kama alivyoniagiza. Kabla sijakamilisha dawa dalili zilisimama. Nilienda kwa daktari na kufanya kipimo kingine cha damu, cha kushangaza nilikuwa hasi. Sijapata dalili tena. Dkt. Dawn ni mzuri na unaweza
    kuwasiliana kwenye WhatsApp: +2349046229159
    Gmail ( dawnacuna314@gmail.com )

    Ikiwa unahitaji dawa za mitishamba kutibu magonjwa yoyote sugu au ya zinaa kama.
    HERPES.
    SARATANI.
    VVU/UKIMWI na zaidi

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FAHAMU JINSI YA KUTOA HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA AU ALIYEPATA MSHTUKO (SHOCK)

VIDONDA VYA TUMBO. (Dalili, Vipimo unavyotakiwa kupima na matibabu yake)